Searching...
Sunday, March 26, 2017

KARIBU NURU EDUCATION CENTRE

Sunday, March 26, 2017

Hiki ni kituo cha watoto wa chekechea ambacho kilianzishwa mwaka 2015, aprili, tarehe 14, na kilianza na wanafunzi 15 na mwaka ulio fuatia watoto walikuwa 20 na kati ya hao wengi wao wamejiunga moja kwa moja darasa la kwanza wakiwa na uwezo mkubwa sana.Na kwa miaka hiyo yote miwili wanafunzi walikuwa wakisoma kwa masaa matatu na nusu tuu,kuanzia saa 2:00 kamili asubuhi hadi saa 5:30 asubuhi.
Mwaka huu wa masomo 2017 kituo kimeweza  kuanzisha mpango wa watoto kusoma kuanzia saa 2:00 asubuhi hadi saa kumi na nusu 10:30 jioni pia hadi siku ya juma mosi ni siku ya shule.
DIRA
Kutoa elimu sahihi na malezi  bora kwa watoto(wanafunzi)  ili kutimiza malengo ya mtoto ,mzazi na jamii kwa ujumla.
DHIMA 
Kufundisha na kuwalea watoto kwa  ustadi mkubwa  na kuibua,kukuza na kuendeleza  vipaji vya watoto kwa kuwatengenezea mazingira sawia kwao.
Kuwafanya watoto wapende shule kwa kuwajengea  ujasili wa kutatua matatizo kama kuepuka kufeli mitihani na woga kwa walimu n.k
WADAU /MARAFIKI WA NUECE
Kukamilisha malengo ya kiutekelezaji kituo kinashirikiana na
Wazazi wa watoto,
Serikali za mitaa, wajasiliamali wadogo na marafiki kama wewe.

SARE YA KITUO Traki nyekundu ,mzura wa kijani na kiatu chochote ila cha kamba vinavyo mfanya mtoto ang’are haswa na kuwa wa  kipekee.

                                                      ANUANI
KIBENA  SHULENI –NJOMBE, kwa mzee Bahari.  SIMU: 0762088103
             0718839483
             0765496770

Barua pepe:   nuecetz@gmail.com                                         asifiwehosea1@gmail.com kihweless@gmail.com




HUDUMA NYINGINEZO.
Tunafundisha twisheni kwa wanafunzi wote wa shule za msingi na sekondari muda wote kwa gharama nafuu kabisa.mfano wakati wa jioni kuanzia saa nane( 8) mchana hadi saa kumi na mbili jioni (12) pia wakati wa rikizo na kwa pre- form one kuanzia mwezi wa nane au watisa na kuendelea.
Tunafundisha ENGLISH COURSE kwa wote
Tunatoa elimu ya ujasiliamali na ushauri pia KIINGEREZA kwa watoto na wakubwa siku ya jumapili kuanzia saa nane8 mchana hadi saa kumi jioni kwa shilingi mia 200 tu.
Tunafanya sherehe mbalimbali  za watoto kama kusherekea siku zao za kuzaliwa (birthday) na mafanikio mengine.
KARIBUNI SANA



    Kibao cha kituo kikiwa katika ukuta wa kibanda cha NGATA ukitokea stendi ya daladala.


                Wanafunzi wa chekechea wakiwa katika michezo yao kituoni.
   Baadhi ya wanafunzi wakiwa kwenye mapumziko na hadithi mbalimbali
  Wanafunzi mchanganyiko wakiwa darasani siku ya jumapili wakijifunza kiingereza kwa bei ileile  ya  sh.200/= tu


   Baadhi ya PRE-FORM ONE baada ya kipindi wakiwa na mwalimu wao wa sayansi 2016
   Katika matukio ya mhimu hatuko nyuma ....hii ni sherehe ya kuzaliwa (birthday) kwa wanafunzi wawili wa katikati Februali, 2017

   Mwalimu wa michezo akiwa na wanafunzi wakiwa kwenye mchezo wa kubashiri..2015

Shukrani za dhati kwenu wote kwa  jitihada mnazozifanya ili kujenga taifa letu.
KARIBUNI SANA NURU

SIMU: 0762088103 
             0718839483 
            0765496770
Share This:

0 comments:

Know us